Перейти к содержимому

ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA DARAJA LA UPADRE SHEMASI FRANCIS MWANANTUMBA - NYANGUGE

Jimbo Kuu la Mwanza | JKM Online tv

0:00 / 0:00

ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA DARAJA LA UPADRE SHEMASI FRANCIS MWANANTUMBA - NYANGUGE

2 032 просмотра · 2 года назад
Jimbo Kuu la Mwanza | JKM Online tv
12,3 тыс. подписчиков
2 032 просмотра · 2 года назад
HOMILIA Ndugu wapendwa, huyu mwana wetu, ambaye ni ndugu na rafiki yenu anaitwa sasa kupewa daraja ya Upadri; fikirini kwa makini ni madaraka gani atakayopewa katika Kanisa. Kweli katika Kristo taifa takatifu lote la Mungu linafanywa kuwa taifa la kikuhani wa kifalme. Lakini yeye mwenyewe Kuhani Mkuu wetu Yesu Kristo aliwateua baadhi ya wanafunzi wake ili watekeleze rasmi katika Kanisa kazi ya kikuhani katika jina lake mwenyewe kwa ajili ya watu. Yeye mwenyewe alitumwa na Baba, naye vilevile aliwatuma Mitume duniani kote, ili kwa njia yao na ya mahalifa wao, yaani Maaskofu, kazi yake ya Mwalimu, Kuhani na Mchungaji iendelee bila kukoma. Na hatimaye, waliwekwa Mapadri wawe washiriki wa urika wa Maaskofu; nao, wakiuunganishwa na Maaskofu katika kazi ya kikuhani, huitwa kwa ajili ya huduma ya taifa la Mungu. Na ndugu huyu baada ya kufikiliwa sana anawekwa sasa katika daraja ya Upadri ili naye apate kuwa mhudumu wa Kristo Mwalimu, Kuhani na Mchungaji, na hivyo kwa kazi yake asaidie kulijenga na kulikuza taifa la Mungu, yaani Kanisa, liwe hekalu lake takatifu. Naye atafananishwa na Kristo aliye Kuhani mkuu na wa milele, na ataunganishwa na ukuhani wa Maaaskofu; yaani atawekwa wakfu kuwa kuhani halisi wa Agano Jipya ill aihubiri Injili, alichunge taifa la Mungu na kuziadhimisha ibada takatifu, hasa sadaka ya Bwana. Nawe, mwana mpendwa sana, utakayewekwa hivi punde katika daraja ya Upadri, tekeleza huduma takatifu ya kufundisha kwa jina la Kristo mwenyewe aliye Mwalimu pekee. Hivyo wagawie wote lile Neno la Mungu ambalo nawe ulilipokea kwa furaha. Unapotafakari sheria ya Bwana angalia usadiki kile unachokisoma, na kufundisha kile unachokisadiki, na kufuasa kile unachokifundisha. Na kwa njia hii, mafundisho yako yawe lishe kwa watu wa Mungu, na manukato ya maisha yako yawe furaha kwa wamwaminio Kristo, ill kusudi kwa neno na kwa mfano upate kuijenga nyumba yaani Kanisa la Mungu. Fanya pia kazi yakutakatifuza katika Kristo. Maana kwa huduma yako sadaka ya kiroho ya waamini itatolewa pasipo kumwaga damu ikiungana na dhabihu ya Kristo ambayo, kwa kufanya umoja na ile ya kwao, itatolewa kwa mikono yako juu ya altare katika adhimisho la mafumbo matakatifu. unachokifanya, Kwa hiyo, elewa vizuri na iga unachokitenda; na kwa kuwa unaadhimisha fumbo la kifo na ufufuko wa Bwana, jitahidi kutiisha viungo vyako kwa kukomesha vilema vyote na kuenenda katika upya wa uzima. Kwa njia ya Ubatizo utaliongezea taifa la Mungu waamini wapya. Kwa sakramenti ya kitubio utasamehe dhambi kwa jina la Kristo na la Kanisa. Kwa Mpako mtakatifu utawafariji wagonjwa; unapofanya ibada takatifu, na katika mfululizo wa saa za siku utamtolea Mungu sala za sifa na shukrani si kwa ajili ya taifa la Mungu tu, bali kwa ulimwengu mzima. Kumbuka kwamba ulitwaliwa katika wanadamu ukawekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo ya Mungu. Hivyo timiza kazi ya kikuhani ya Kristo kwa furaha ya daima na katika upendo wa kweli, ukiyatafuta si mambo yako mwenyewe, bali ya Yesu Kristo. Na hatimaye, mwana mpendwa sana, kwa upande wako fanya kazi ya Kristo Kiongozi na Kuhani chini ya Askofu na katika ushirika naye; ujibidishe kuwakusanya waamini katika familia moja ili upate kuwaongoza kwa Mungu Baba kwa njia ya Kristo na katika Roho Mtakatifu. Ndiyo maana, umkazie daima macho yako Yesu Kristo aliye Mchungaji mwema, ambaye hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.