WAZIRI MKUU AKUTANA NA MADUDU BWALO LA MILIONI 774, AMSIMAMISHWA KAZI MHANDISI, PESA HAZIONEKANI
Cg Online Tv
0:00 / 0:00
WAZIRI MKUU AKUTANA NA MADUDU BWALO LA MILIONI 774, AMSIMAMISHWA KAZI MHANDISI, PESA HAZIONEKANI
620 просмотров · 2 года назад
Cg Online Tv
97,4 тыс. подписчиков
620 просмотров · 2 года назад
#CgOnlineTv #Majaliwa #Iringa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, Emmanuel Sigachuma ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Lugalo.
Pia amempa onyo kali Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri hiyo Nelson Milanzi kufuatia ubadhirifu huo.
Katika mwendelezo wa ziara yake ya kikazi mkoani Iringa, Waziri Mkuu Majaliwa pia ameagiza kutafutwa popote alipo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kilolo, Laini Kawendu ili naye ajibu tuhuma hizo na sheria ichukue mkondo wake.
Akiwa katika shule hiyo ya Sekondari ya Wasichana ya Lugalo kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule hiyo, Waziri Mkuu Majaliwa ameshangaa hatua ya kutumika kwa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa Bwalo lakini mpaka sasa halijakamilika.
Bwalo hilo lilipangiwa kutumia shilingi Milioni 774 hadi kukamilika kwake na mpaka sasa ujenzi huo umetumia shilingi Milioni 341 ukiwa umefikia hatua ya linta ambayo ni sawa na asilimia 40 ya ujenzi wake