WANANCHI KUSHIRIKISHWA KUONDOLEWA NGARESERO, PORI TENGEFU
CLOUDSMEDIA
0:00 / 0:00
WANANCHI KUSHIRIKISHWA KUONDOLEWA NGARESERO, PORI TENGEFU
1 473 просмотра · 3 года назад
CLOUDSMEDIA
1,55 млн подписчиков
1 473 просмотра · 3 года назад
Serikali imesema kuwa itashirikisha wananchi kuhusu utekelezaji wa Maamuzi ya Baraza la Mawaziri ya kukiondoa Kijiji cha Ngaresero katika Pori Tengefu la Ziwa Natron kutokana na sababu kwamba Pori hilo ni moja kati ya maeneo yaliyotolewa maelekezo na Baraza la Mawaziri kuwa lipandishwe hadhi.
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro, Mhe. Emmanuel Lekishon Shangai, lililoulizwa na Mhe. Zaytun Swai kuhusu lini Serikali itaondoa Kijiji cha Ngaresero kwenye eneo la Pori Tengefu la Pololet baada ya kujumuishwa kimakosa.