BWANA NI MCHUNGA - Mzizima SDA Choir Ft. Faraja Ernest (official Video 4K)
MZIZIMA SDA CHURCH
0:00 / 0:00
BWANA NI MCHUNGA - Mzizima SDA Choir Ft. Faraja Ernest (official Video 4K)
16 188 просмотров · 1 год назад
MZIZIMA SDA CHURCH
2,78 тыс. подписчиков
16 188 просмотров · 1 год назад
Kama kondoo asiye na Mchunga tulitanga mbali na Bwana. Kwa wingi wa wema na fadhili zake, Mungu, Mchunga Mwema aliturejesha zizini.
Si zamani pekee tulipomuhitaji atuokoe, hata sasa tunahitaji kuchungwa naye tusipotee milele. Furaha gani kumsikia Yesu akijitambulisha kwetu kama Mchungaji, tena Mchungaji mwema, na njia ya kweli na uzima?
Ni sasa ambapo twahitaji kumwandama kila aendako maana atuongoza mahali salama penye pendo na utulivu wa milele. Hapo tutaketi daima.
Bwana Mchunga Mwema / The Lord's My Shepherd
Lyrics: James Montgomery
Music: Thomas Koschat
Translation: Nyimbo za Kristo 132
Audio: Bjbrand studios
Video: Marcko zacky
Instrumentation: Jacob Mang'ombe
Lyrics
Bwana ni mchunga, sitahitaji.
Majani mabichi malisho yangu.
Ananinywesha maji matulivu.
Atanirudisha nikipotea.
Nipitapo bondeni mwa mauti.
U mlinzi wangu sitaogopa.
Fimbo yako yatosha kunilinda.
Ukinifariji sina hasara.
Kati ya mateso meza waanda.
Na kikombe changu kinafurika.
Umenipaka kichwani mafuta.
Nitaulizaje zaidi kwako?
Wema na fadhili zinifuate.
Siku zangu zote hata milele.
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana.
Katika ufalme wa pendo lake.
©Mzizima SDA Choir 2024
#hymns #sdahymns #christianhymns #sdachurch