Перейти к содержимому

MAKALA: UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO, HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE, NJOMBE

WANGING'OMBE DISTRICT COUNCIL

0:00 / 0:00

MAKALA: UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO, HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE, NJOMBE

322 просмотра · 1 год назад
WANGING'OMBE DISTRICT COUNCIL
24 подписчика
322 просмотра · 1 год назад
HALMASHAURI ya Wilaya ya Wanging’ombe ni miongoni mwa halmashauri sita (6) zinazounda Mkoa wa Njombe. Halmashauri imeanzishwa mwezi machi 2012 kabla hapo ilikuwa sehemu ya Wilaya ya Njombe Vijijini. Jina Wanging’ombe limetokana na jina la kijiji cha Wanging’ombe ambacho kipo katika kata ya Wanging’ombe tarafa ya Wanging'ombe. Makao makuu ya Wilaya na Halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe ipo kijiji cha Chalowe katika kata ya Igwachanya. Wilaya ya wanging’ombe ina ukubwa wa eneo lenye Kilomita za Mraba 3,570, ikiwa na watu 191,506 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022. Wakazi wa wilaya ya Wanging’ombe ni Wabena, wakinga, wahehe na watu wa makabila tofauti tofauti. Wilaya ya Wanging’ombe ina Tarafa 3, Kata 21 na Vijiji 108 na vitongoji 525. Ikolojia ya Wilaya ya Wanging’ombe imegawanyika katika makundi mawili kuna maeneo ni ya ukanda wa baridi na ukanda wa joto. Kutokana na ilkolojia hiyo wakazi wa Wanging’ombe wanajishughulisha na shughuli za kilimo cha mazao ya chakula ambayo ni mahindi, mtama, viazi mviringo, viazi vitamu, maharage, mihogo, njugu mawe, ngano, kunde na njegere na mazao ya biashara kama vile kahawa, chai, alizeti, pareto na karanga pamoja na Ufugaji. Pamoja na shughuli za kilimo wakazi wa wanging’ombe pia wanajishughulisha na ufugaji wa nyuki, ufugaji wa Ng’ombe, Mbuzi, Kuku pamoja na biashara ndogondogo.