RAIS Mwinyi aicharukia ZAECA baada ya CAG kuonyesha watumishi wa SMZ walivyoiba mabilioni ya umma
Zanzibar Kamili TV
0:00 / 0:00
RAIS Mwinyi aicharukia ZAECA baada ya CAG kuonyesha watumishi wa SMZ walivyoiba mabilioni ya umma
14 851 просмотр · 4 года назад
Zanzibar Kamili TV
85,7 тыс. подписчиков
14 851 просмотр · 4 года назад
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi ameagiza kuchukuliwa hatua kwa watendaji wote waliohusishwa na ubadhirifu wa mali za umma na uhujumu uchumi katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Zanzibar (CAG) ya mwaka wa fedha 2020/2021.
Hayo ameyasema leo baada ya kupokea ripoti ya taarifa ya CAG katika viwanja vya Ikulu Zanzibar.
Katika maelezo yake Rais Dk.Mwinyi ameitaka Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) kujitathmini upya kiutendaji, pia Rais Dk.Mwinyi ameitaka Mamlaka hiyo kuifanyia kazi ripoti iliyowasilishwa yenye taarifa za upotevu wa fedha.