MWANZO MWISHO WALIVYOACHIWA WAFUNGWA GEREZA LA BUTIMBA MWANZA KWA MSAMAHA WA RAIS MAGUFULI
GSengo
0:00 / 0:00
MWANZO MWISHO WALIVYOACHIWA WAFUNGWA GEREZA LA BUTIMBA MWANZA KWA MSAMAHA WA RAIS MAGUFULI
6 822 просмотра · 6 лет назад
GSengo
59,2 тыс. подписчиков
6 822 просмотра · 6 лет назад
Siku moja baada ya Rais wa Tanzania, John Magufuli kuwasamehe wafungwa 5,533 katika maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, wafungwa 79 kati ya hao waliokuwa wamefungwa katika gereza la Butimba Mkoa wa Mwanza wameachiwa Jumanne Desemba 10, 2019.
Rais Magufuli alitangaza msamaha huo katika maadhimisho hayo, akibainisha kuwa idadi hiyo ni kubwa kuwahi kutokea kuliko wakati mwingine wowote na kutaka walengwa ndio waachiwe.
Katika mkoa wa Mwanza wafungwa watakaopata msamaha huo ni 190.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amefika katika gereza la Butimba kwa ajili ya kushuhudia utekelezaji wa agizo la Magufuli huku mkuu wa gereza hilo, Hamza Hamza akitaja idadi ya watakaoachiwa.