WAKAZI WA KATERERO NA IBWELA KUNUFAIKA NA DARAJA LA KALEBE, KAGERA
Wizara ya Ujenzi
0:00 / 0:00
WAKAZI WA KATERERO NA IBWELA KUNUFAIKA NA DARAJA LA KALEBE, KAGERA
255 просмотров · 9 дней назад
Wizara ya Ujenzi
9,24 тыс. подписчиков
255 просмотров · 9 дней назад
Wakazi wa maeneo ya Katerero na Ibwela mkoani Kagera wanatarajia kunufaika na Daraja la Kalebe, ambalo limejengwa ili kurahisisha usafirishaji na kuimarisha mawasiliano kati ya wilaya za Bukoba, Muleba na Karagwe.
Daraja hilo linatarajiwa kuwa suluhisho kwa wakazi na wafanyabiashara, hususan katika kusafirisha mazao ya biashara kwenda katika masoko mbalimbali. Awali, watumiaji wa eneo hilo walikabiliwa na changamoto kubwa kutokana na daraja la zamani kushindwa kupitika, hasa wakati wa msimu wa mvua.
Msimamizi wa ujenzi wa mradi wa Daraja la Kalebe, Mhandisi Kenneth Mkude, amesema daraja hilo jipya lina urefu wa mita 60 na upana wa mita 11.