TANROADS: ULINZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA NA MADARAJA NI JUKUMU LA KILA MWANANCHI
Wizara ya Ujenzi
0:00 / 0:00
TANROADS: ULINZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA NA MADARAJA NI JUKUMU LA KILA MWANANCHI
354 просмотра · 2 месяца назад
Wizara ya Ujenzi
9,24 тыс. подписчиков
354 просмотра · 2 месяца назад
📌 Kamera Kufungwa Kudhibiti Uharibifu
Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Kigoma imetoa rai kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa miundombinu ya barabara kushiriki kikamilifu katika kulinda na kutunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kuendelea kuwa salama kwa watumiaji.
Rai hiyo imetolewa na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Elsony Mweladzi, ambaye amesema kuwa mkoa huo una jumla ya madaraja 396, yakiwemo madaraja makubwa matano ambayo yote yako katika hali nzuri na salama kwa matumizi ya wananchi.
Mhandisi Mweladzi amesema ni muhimu wananchi kutunza na kulinda uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika miundombinu ya barabara na madaraja ili kuepusha hasara zinazoweza kujitokeza kutokana na vitendo vya uharibifu.