SITA WAUAWA BAADA YA WANAKIJIJI KUVAMIA ASKARI
ITV Tanzania
0:00 / 0:00
SITA WAUAWA BAADA YA WANAKIJIJI KUVAMIA ASKARI
3 049 просмотров · 8 часов назад
ITV Tanzania
1,37 млн подписчиков
3 049 просмотров · 8 часов назад
Watu sita, akiwemo Afisa mmoja wa Wanyamapori, Askari wa TAWA, walinzi wawili wa Hifadhi za Vijiji (VGS) na madereva wawili, wameuawa baada ya kundi linalodaiwa kuwa la wafugaji kuvamia kambi ya askari wa doria katika Hifadhi ya Wanyamapori Iswagala, Kijiji cha Utimle, Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora, tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Septemba 18, 2026, baada ya kufanyika kwa oparesheni ya kukamata mifugo iliyoingia hifadhini kinyume cha sheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi wa Polisi Twaha Lulengelule, amesema kundi hilo linadaiwa kuvamia kambi hiyo na kuwashambulia kwa kutumia silaha za jadi watumishi waliokuwa wakitekeleza majukumu ya doria.
Aidha, watu wengine watano kutoka upande wa hifadhi wamejeruhiwa katika tukio hilo.
Kwa taarifa zaidi ufuate (follow) ukurasa wetu
Powered by #MCHEZOSUPA
JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
-
Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
#ITVDigital #ITVUpdates ITVTanzania
Follow @itvtz @radioonetanzania
@capitaldigitaltanzania